Header Ads Widget

Recent in Sports

test

TAFINA YAZINDULIWA RASMI

Na Mwandishi Wetu.

Katika kuunga mkono juhudi za serikali kwenye sekta ya UWEKEZAJI Nchini , Mtandao wa UMOJA WA WANACHAMA WANAOTOA HUDUMA ZA KIFEDHA KUPITIA TEKNOLOJIA ( TANZANIA FINTECH ASSOCIATION - TAFINA ) wamejipanga kuhakikisha wanawaongezea mitaji wadau wa Maendeleo na kuweka mazingira rafiki ya Kisera ili kuvutia wawekezaji katika kuboresha maisha ya Watanzania na kuwainua kiuchumi .


Kennedy Komba, Mkurugenzi wa Ukuzaji na Ushirikishwaji wa Fedha Benki Kuu Ya Tanzania (BoT) na Mwenyekiti wa TAFINA Cynthia Ponera baada ya uzinduzi huo.

Ameyasema hayo Katibu Mkuu wa TAFINA , Shadrack Kamenya , Leo Machi 01 , 2024 katika Uzinduzi wa TAFINA uliofanyika Jijini Dar Es Salaam , ambapo amebainisha kuwa dhima kubwa ya uanzishaji wa TAFINA ni kuhakikisha kunakuwepo na Umoja wa Watoa Huduma .


Aidha , Bwn. Shedrack ameongezea kuwa Umoja huu tayari una Wanachama zaidi ya 50 na wamejipanga kutoa huduma bora na rafiki kwa watanzania pamoja na kufuta misingi yote ya Kisheria .


Kwa upande wao wanachama wa TAFINA wamesema umoja huu utawasaidia katika kushirikiana na kubadilisha mawazo , kuendeleza biashara na uwekezaji mbalimbali Nchini.

Tanzania Fintech Association (TAFINA) iliyosajiliwa Machi 2023 ina furaha kutangaza uzinduzi wake rasmi, chama chenye nguvu na jumuishi kinacholenga kukuza uvumbuzi, ushirikiano na ukuaji ndani ya sekta ya teknolojia ya fedha.

TAFINA iliibuka kama jibu la hitaji linalokua la jukwaa moja ambalo linatetea maslahi ya wabunifu wa fintech na wadau nchini Tanzania. Kwa maono ya kukuza, kukuza na kuwezesha mfumo ikolojia wa fintech nchini Tanzania, chama kitatumika kama kichocheo cha maendeleo, kuwezesha wanachama kujiinua kwenye utaalamu wa pamoja, rasilimali, mitandao ili kuunda mustakabali wa fedha.

TAFINA YAZINDULIWA RASMI TAFINA YAZINDULIWA RASMI Reviewed by Adery Masta on March 01, 2024 Rating: 5

No comments:

Powered by Blogger.